Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kampuni yashusha neema kwa wakulima wa tumbaku Tabora
Habari Mchanganyiko

Kampuni yashusha neema kwa wakulima wa tumbaku Tabora

Spread the love

 

KAMPUNI ya Mkwama imejitosa katika ununuzi wa zao la tumbaku mkoani Tabora na kuwataka wakulima wa mkoa huo kulima kwa wingi zao hilo kwa sababu sasa soko lipo la uhakika. Anaripoti Paul Kayanda, Tabora … (endelea).

Kampuni hiyo imetamba kuwa imejipanga katika ushindani wa masoko na tumbaku yote itanunuliwa.

Hayo yameelezwa jana tarehe 25 Aprili 2023 na Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Ahmed Mansoor Huwel wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Tabora baada ya uzinduzi wa masoko ya tumbaku kwenye maghala yake yaliyozinduliwa na mkuu wa mkoa wa Tabora, Balozi Dk. Batilda Burian.

Aidha, alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuikaribisha kampuni hiyo ya mzawa kwenye sekta ya tumbaku huku Waziri wa Kilimo, Husein Bashe akiwapa nguvu wanunuzi wa zao hilo ili kuwasaidia wakulima hao.

Alisema kuwa ili kuendelea kusaidia na kunyanyua wakulima wametumia zaidi ya Sh milion 45 kufufua na kuwasha kiwanda cha tumbaku Morogoro licha ya kwamba mwaka jana walikuwa wageni katika biashara hiyo.

“Nachotaka kusema wakulima wote warudi waende mashambani Mkwawa tumejipanga vizuri, masoko ni yakutosha kwa hiyo tutashawishi wakulima kurudi mashambani na niombe sana kwa walioacha kulima tumbaku warudi kampuni yao ya mzawa imerudi nyumbani kukomboa wakulima,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

error: Content is protected !!