RAIS Samia Suluhu Hassan amesema miaka 59 ya Muungano imekuwa yenye umoja, amani na ustawi wa Taifa kama ilivyokuwa ndoto za waasisi wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam …(endelea).
Rais Samia ametoa ujumbe huo leo Jumatano tarehe 26 Aprili 2023 wakati Tanzania ikiadhimia miaka 59 ya muungano tangu kuasisiwa kwake mwaka 1964 na Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere pamoja na Mzee Abeid Amani Karume.
Kupitia mtandao wa Twitter, Rais Samia amendika hivi; “Nawatakia nyote kheri tunapoadhimisha Miaka 59 ya Muungano. Imekuwa miaka 59 ya Umoja, yenye Amani na Ustawi, kama ilivyokuwa ndoto ya waasisi wetu, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume. Tuendelee kuidumisha tunu hii adhimu na ya kipekee kwa Taifa letu.”
Nawatakia nyote kheri tunapoadhimisha Miaka 59 ya Muungano. Imekuwa miaka 59 ya Umoja, yenye Amani na Ustawi, kama ilivyokuwa ndoto ya waasisi wetu, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume. Tuendelee kuidumisha tunu hii adhimu na ya kipekee kwa Taifa letu.
— Samia Suluhu (@SuluhuSamia) April 26, 2023
Maadhimisho hayo ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, safari hii yanafanyika kimkoa kama ambavyo Rais Samia alivyoagiza kwamba yafanyike katika ngazi ya mikoa kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi.
Tarehe 15 Aprili 2023 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Jumamosi wakati alizindua Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 Zanzibar, alisema Rais Dkt. Samia ameelekeza shughuli za maadhimisho hayo zifanyike kuanzia tarehe 17 Aprili, 2023 hadi siku ya kilele tarehe 26 Aprili, 2023.
Alisema kuwa maadhimisho hayo ambayo yatafanyika kupitia mikoa, taasisi za serikali na vyombo vyote vya ulinzi na usalama yaambatane na uzinduzi wa miradi ya maendeleo, shughuli za kijamii hususan upandaji miti, usafi wa mazingira na mashindano ya michezo na sanaa mbalimbali.
Sandarusi ngapi kumridhisha MTOA HOJA… KUWA HOJA YAKE MOJA NI TAASISI AU INAITAJI ZAIDI YA DORA ZA MAREKANI TRILION 3452653 KUMRIDHISHA PAMOJA NA URAIS JUU..
https://jiji.co.tz/houses-apartments-for-sale