Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Jicho la Rais Magufuli lahamia kwa wastaafu hewa
Habari za Siasa

Jicho la Rais Magufuli lahamia kwa wastaafu hewa

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amewataka watendaji katika mifuko ya hifadhi ya jamii kuboresha daftari la orodha ya majina ya wastaafu, ili kuondoa mapungufu yaliyopo pamoja na kudhibiti uwepo wa wastaafu hewa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Dk. Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 28 Desemba 2018 wakati akizungumza na viongozi wa vyama vya wafanyakazi na mifuko ya hifadhi ya jamii, akisema kuwa kama serikali iliwahi kubaini juu ya uwepo wafanyakazi, wanafunzi, mishahara na pembejeo hewa, haiwezi kukosa wastaafu hewa.

“Niwaombe, kwenye mifuko sababu katika mifuko hii waboreshe daftari la wastaafu ili kuondoa wastaafu hewa au usajili wa kujirudia,  kama tumekuwa na wastaafu hewa, pembejeo hewa mishahara hewa, wanafunzi hewa, hatuwezi tukakosa wastaafu hewa, lazima tunao. Hatuwezi tukakosa wastaafu ambao wameandikwa majina mara mbili,” amesema Rais Magufuli.

Katika agizo lingine, Rais Magufuli ameitaka mifuko ya hifadhi ya jamii kupunguza matumizi ya ovyo pamoja na uwekezaji wa miradi isiyo na tija, ili iwe na uwezo wa kulipa mafao ya wastaafu kwa wakati na kiwango kinachotakiwa.

“Mnafahamu hata mifuko hii ilikuwa inaendeshwa kiajabu, pakawa panaanzishwa miradi ya ajabu ajabu na mingi ilikuwa ya majengo, nenda kigamboni uangalie majengo yaliyojengwa, fikiria aliyeweka mabilioni ya fedha alitegemea ataingiza kiasi gani.

“Sina uhakika kama mlikuwa mnaamua mnataka miradi ya aina hii, walikuwa wanaamua watendaji pasipo kushirikisha wafanyakazi,” amesema na kuongeza Rais Magufuli.

“Uwekezaji usio na tija usifanyike,  tupunge gharama za uendeshaji wa mifuko, sababu sasa hivi imebaki mifuko mwili hakuna sababu za kushindana, huu ni mfuko wa sekta binafsi na huu wa umma ina wanachama wake,

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!