JAJI mwandamizi wa Mahakama ya Juu nchini Pakistani Jaji Qazi Faezi Isa ameshangazwa na matendo ya Magaidi kwa kushindwa kuelewa wanapata nini kutoka kwa nani. Anaripoti Mwandishi wetu … (endelea).
Akizungumza katika mkutano wa 9 wa mahakama ulioandaliwa na Tume ya Sheria na Haki ya Pakistan katika Jengo la SC Jumamosi, Jaji Isa aliuliza ni ofa gani zinazotolewa kwa ajili ya magaidi.
“Je, tunawaambia ‘tafadhali piga shule tano na sio sita na tafadhali chukua pesa na silaha’,” alisema kwa kejeli, kabla ya kuuliza ni wapi mazungumzo yanafanyika na ni nani aliyeidhinisha.
Jaji Isa alisema kuwa uislam unahimiza kusoma na kwamba aya ya awali iliyoshushwa kwenye Quran ilihimiza elimu inakuaje Magaidi wanakinzana na elimu.
Jaji pia alisikitika kwamba uhakika takwa la kikatiba wa haki ya kuishi na elimu ya lazima kwa kila mtu umeshambuliwa nchini Pakistan.
“Mazungumzo pekee ambayo Mwislamu wa kweli atakuwa nayo ni kuwaletea Qurani Tukufu na Sunnah,” alionya, akiongeza kwamba amri ya kwanza ya Mwenyezi Mungu katika Quran Tukufu alikuwa “Iqra” (soma).
Alinukuu data za matukio ya kigaidi ulimwenguni kutoka mwaka 1970 hadi 2019, alisema kulikuwa na mashambulio 1,000 kwenye taasisi za elimu nchini humo.
Jaji Isa pia aligusia masuala kama vile mauaji ya heshima na mabadiliko ya hali ya hewa.
Akiita sheria dhidi ya mauaji ya heshima ‘dead letter,’ alisikitika kuwa sheria ipo lakini haitekelezwi.
“Hii ni moja ya sheria chache ambazo zimetolewa moja kwa moja kutoka kwa Qur’ani Tukufu na inashughulikia kosa la Qazf,” aliongeza.
Aliulizwa kuhusu kurugenzi mpya ya sheria iliyoanzishwa katika Makao Makuu yenye jukumu la kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kisheria kuhusu sheria za kimataifa na Katiba.
Katika jibu lake, jaji huyo alisema hafahamu kurugenzi yoyote kama hiyo lakini yuko ‘tayari zaidi’ kutoa ujuzi wake wa Katiba na sheria iwapo ataalikwa. Jukumu la wanawake katika kufanya maamuzi Pakistani
Wakati huo huo, Jaji Mkuu Umar Ata Bandial alivitaka vyombo mbalimbali vya dola kuhakikisha ushirikishwaji wa wanawake katika mchakato wa kufanya maamuzi na akataka juhudi za kutokomeza ukatili wa kijinsia na upendeleo mwingine rasmi na usio rasmi unaowakabili wanawake nyumbani na sehemu za kazi.
Katika hotuba yake ya kuhitimisha mkutano huo, alisisitiza umuhimu wa kufanya mahakama ziwe rahisi kwa wananchi wote, bila kujali jinsia zao, dini, rangi na hali zao kiuchumi.
Alisisitiza matumizi ya teknolojia na kuwataka wadau katika mfumo wa haki ya jinai – polisi na waendesha kuboresha utendaji wao na uratibu wao kwa wao.
Leave a comment