Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari Hospitali ya Aga Khan matatani, Polisi waichunguza
Habari

Hospitali ya Aga Khan matatani, Polisi waichunguza

Spread the love

 

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam nchini Tanzania, linaichunguza Hospitali ya Aga Khani, jijini Dar es Salaam, kwa tuhuma za kutoza gharama kubwa za matibabu. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea)

Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema leo Alhamis, tarehe 18 Februari 2021 kuwa, wamepokea malalamiko kutoka kwa wananchi dhidi ya hospital hiyo.

Mambosasa amesema, malalamiko hayo yanahusu “kutoza gharama kubwa za matibabu kwa wagonjwa wa matatizo kifua (Pneumonia) ambayo hupelekea matatizo ya upumuaji.”

SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Kanda Maalum Dar es Salaam

“Aidha wagonjwa wanaopatiwa matibabu katika hospitali hiyo, pindi wanapofariki dunia kumekuwa na tabia ya kuzuia miili ya marehemu na kudai kiasi kikubwa cha fedha kinyume na maelekezo ya Serikali kupitia wizara ya afya maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto,” amesema Mambosasa

Kamanda huyo amesema “menejimenti ya hospital hiyo, inatabia mbaya ya kuzuia miili ya marehemu na baada ya kuzuia, wanalazimisha sasa kutoza bili kubwa ambayo haziendani na tiba ambazo mgonjwa alikuwa hapati.”

Wamekuwa wakifanya hivyo kwa muda mrefu na kuwafanya wahusika kwenda kuuza vitu ili waje kulipa hali ambayo ni kinyume na utaratibu wa wizara ya afya.

Amesema, baada kupokea malalamiko hayo, limefungua jalada la uchunguzi lenye kumbukumbu namba DSMZ/CID/PE/34/2021 dhidi ya malalamiko hayo.

“Uchunguzi huu utakapokamilika na kubaini tuhuma hizi hatua kali za kisheria zitachukuliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama na wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto dhidi ya hospitali hiyo,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!