Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Tangulizi NEC yamteua diwani NCCR-Mageuzi
Tangulizi

NEC yamteua diwani NCCR-Mageuzi

Spread the love

 

TUME ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania (NEC), imemteua Renatha Lihange Mizungo, kuwa Diwani Viti Maalumu kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, Kigoma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo Alhamisi tarehe 18 Februari 2021 na Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Dk. Wilson Mahera.

Kwenye taarifa hiyo, Dk. Mahera amesema, uteuzi huo umefanyika kwa mujibu wa sheria ya serikali za mitaa, baada ya Chama cha NCCR-Mageuzi kupata madiwani wawili katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, Kigoma kwenye Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020.

“Kifungu cha 35(1) (C) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura ya 287 kifungu cha 19 (1) (C) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), sura ya 288 pamoja na kifungu cha 86A cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, sura ya 292 vinaweka takwa la kuwa na madiwani wanawake wa viti maalumu wasiopungua theluthi moja ya wajumbe wote wa halmashauri husika,” imesema taarifa ya Dk. Mahera.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dk. Wilson Mahera

Taarifa ya Dk. Mahera imesema “hivyo, NEC hufanya uteuzi wa madiwani wanawake wa viti maalumu katika halmashauri zote nchini.”

“Kwa kuzingatia ushindi wa chama husika, katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, NCCR-Mageuzi katika Halmashauriya Kasulu kilipata madiwani wawili,” imeeleza taarifa hiyo.

Mkurugenzi huyo wa uchaguzi NEC, amesema uteuzi huo umefanyika baada ya tume hiyo kupokea barua ya utambulisho wa Mizungo, kutoka kwa Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi.

“Baada ya kupokea fomu namba 8E kutoka kwa Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, iliyowasilishwa kwa barua yenye Kumb. Na. NCCR-M/MM/TV/15/125 ya tarehe 5 Februari 2021, tume katika kikao chake cha tarehe 17 Februari 2021 ilipitia na kukagua fomu hiyo,” imesema taarifa ya Dk. Mahera na kuongeza.

“Na baada ya kujiridhisha imemtea ndugu Renatha Lihange Mizungo kuwa Diwani wa Viti Maalum katika Halmashauyri ya Wilaya ya Kasulu kupitia chama cha NCCR-Mageuzi.”

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!