Waziri wa Katiba na Sheria, Damas Ndumbaro, ameeleza umuhimu wa Chama cha Mawakili wa Serikali kwa kueleza majukumu yao kuwa mazito na muhimu kwa serikali. Anaripoti Urumasalu Kisung’uda, TUDARCo … (endelea)
Katika Mkutano Mkuu wa Chama cha Mawakili wa Serikali tarehe 29 Septemba 2022 Mkoani Dodoma wenye lengo la kuzindua Chama cha mawakili Ndumbalo amesema Wanasheria wanahusika na utoaji haki, usimamizi wa sheria, tafsiri za sheria, kusuluhisha migogoro katika kutia sahihi na mikataba.
Amesema chama hicho kitashughulika na masuala ya kitaaluma , maadili ya wanasheria kwa kutoa changamoto za kimaadili zinazowakabili.
“Pia chama hiki cha mawakili kinatarajiwa kuleta umoja wenye nguvu na jukwaa mahususi la kushauri Serikali katika kazi zake, vilevile jukwaa hilo litakuwa sehemu ya majadiliano kati ya wanasheria kwa Serikali ambayo haikuwepo kabla,” amesema Ndumbaro.
Ndumbalo amesema chama hiki kitakuwa eneo la kuwasilisha mawazo ya wanachama yanayoathiri taaluma yao kwa namna moja au nyingine.
“Chama hiki ni sehemu ya kuimarisha mfumo wa sheria ambao unaathiri sekta ya sheria katika utumishi wa umma, pia utasimamia na kuendesha mafunzo mbalimbali ya mawakili walioko katika utumishi wa umma,” amesema Ndumbaro.
Leave a comment