Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yabariki mazungumzo ya Rais Samia, Lissu
Habari za Siasa

Chadema yabariki mazungumzo ya Rais Samia, Lissu

Spread the love

 

 CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema mazungumzo aliyofanya Makamu Mwenyekiti wake Bara, Tundu Lissu na Rais Samia Suluhu Hassan, jijini Brussels, Ubelgiji ni ya chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Ijumaa, tarehe 18 Februari 2022 na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

“Sisi ni waumini wa mazungumzo, kwa maana nyingine  mazungumzo aliyoyafanya Lissu ni mazungumzo ya chama. Lakini tutazungumza na tunaozungumza nao tunawataka wakati wote,  waweke unafiki pembeni wasimamie ukweli na haki katika mazungumzo,” amesema Mnyika.

Hata hivyo, Mnyika amesema, Chadema kinapofanya mazungumzo na Serikali, haiwazuii kuendelea na mapambano.

“Lakini kushiriki kwetu mazungumzo na milango yetu iko wazi, ya mazungumzo lakini hatuzuiwi kuendelea na mapambano ya njia nyingine za demokrasia.,” amesema Mnyika.

Katibu Mkuu huyo wa Chadema, amesema wanasubiri Rais Samia atimize ahadi yake aliyoitoa bungeni mwaka jana, ya kufanya mazungumzo rasmi na chama hicho.

“Tutashiriki mazungumzo wakati wote tutakapoona yanaleta matokeo. Mimi kwa imani yangu kwa upepo uliotoeka leo, Rais akirejea Tanzania, bado atatimiza ahadi yake aliyoitoa bungeni kwamba atafanya mazungumzo nasi,” amesema Mnyika na kuongeza:

“Tunasubiri kuendelea na mazungumzo awamu ya pili, mpaka kieleweke.”

Rais Samia alifanya mazungumzo na Lissu, juzi Jumatano, ambapo alipokea maombi matano kutoka kwa makamu mwenyekiti huyo wa Chadema, aliyoahidi kuyafanyia kazi.

Miongoni mwa mambo hayo, ni kesi ya ugaidi, inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe na wenzake, katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Dar es Salaam.

Mengine ni upatikanaji wa katiba mpya, tume huru ya uchaguzi na ondoleo la zuio la mikutano ya vyama vya siasa vya upinzani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!