Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema wajifungia kujadili mustakabali wa DP World
Habari za Siasa

Chadema wajifungia kujadili mustakabali wa DP World

Spread the love

KAMATI Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imekutana kujadili hali ya kisiasa nchini, ikiwemo mkataba wa ushirikiano kuhusu uendeshaji bandari, ulioingia baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam… (endelea).

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, wakati akizungumza na wandishi wa habari kuhusu ajenda zitakazojadiliwa katika kikao cha kamati hiyo kilichoketi leo Jumamosi, jijini Dar es Salaam.

Mbali na kujadili mkataba wa bandari, Mnyika amesema kikao hicho kitajadili mazungumzo kati ya Chadema na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Kikao cha Kamati Kuu kina ajenda mbalimbali, muda huu tunaendelea na ajenda ya taarifa ya hali ya kisiasa ikiwepo mkataba wa bandari na mazungumzo kati ya Chadema na CCM,” amesema Mnyika.

Serikali ya Tanzania, kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Serikali ya Dubai, kupitia kampuni yake ya Dubai Port World, imeingia makubaliano ya kuendesha bandari nchini, ambao umeibua mjadala mkali kwa baadhi ya watu kudai baadhi ya vifungu vyake vinakiuka maslahi ya taifa.

Miongoni mwa hoja zikizoibuliwa na wanaopinga mkataba huo, ni kutokuwa na Muda mahususi wa utekelezaji, kuwa na kifungu kinachozuia mkataba huo kuvunjwa, pamoja na kutoanisha maslahi ambayo nchi itapata.

Hata hivyo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, jana Ijumaa aliwatoa hofu wananchi akisema mkataba huo ni wa awali na kwmaba kuna kipengele kinachoruhusu kuvunjika endapo kutatokea dosari yoyote.

Pia, Waziri Majaliwa alisema Serikali haijauza bandari, badala yake imetafuta mwekezaji kama ilivyofanyika katika Kampuni ya TICS na kwamba DP World kupitia mikataba ya utekelezaji miradi itakayoingiwa itapewa Muda wa utekelezaji kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake.

Waziri Majaliwa alisema DP World haitapewa bandari zote bali ni baadhi ya sehemu katika bandari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!