CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema hakitawabeba viongozi mizigo katika chaguzi zijazo, huku kikiwataka waliopewa dhamana wakati huu kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kujenga imani kwa wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Rukwa … (endelea).
Onyo hilo limetolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Idara ya Oganaizesheni, Issa Ussi Gavu, akizungumza na wananchi pamoja na viongozi wa chama hicho Wilaya ya Nkasi, mkoani Rukwa.
“Niwaombe sana wetu nendeni mkatimize wajibu wenu na sisi kama CCM hatutakuwa tayari kumbeba, kumsaidia au kuhakikisha kwamba mtu asiyetimiza wajibu wake sisi tunamtia kwenye mbeleko. Umbeleko wa CCM utambeba kiongozi aliye tayari kujitoa, kutenda na kuwatumikia anaowaongoza,” amesema Gavu.
Gavu amewataka wenyeviti wa vitongoji, vijiji na mitaa wakatekeleze majukumu yao kwa mujibu wa sheria, huku akiwasisitiza kutoa taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi wao ili kuwaondoa mashaka juu ya matumizi ya mapato.
“Mnatakiwa muitishe vikao vya mapato na matumizi kwenye maeneo yenu ili wananchi wapate taarifa zilizo sahihi, kilichopatikana, kilichotumika, faida na kasoro zake ili kupunguza mashakama kwa jamii unayoiongoza na kujenga imani na upendo kwako pamoja na chama na serikali,” amesema Gavu.
Leave a comment