MWANAHARAKATI huru, Bihimba Mpaya ametoa msaada wa mifuko ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madrasa iliyopo katika msikiti wa Aisha, Kivule jijini Dar es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Bihimba ametoa msaada huo jana tarehe 26 Januari 2024, baada ya swala ya Ijumaa iliyofanyika msikitini hapo, jijini Dar es Salaam.
“Namshukuru Mungu leo tumeswali pamoja katika msikiti huu uliopo eneo la Mgambo Mtaa wa Kivule. Nimetoa saruji mifuko 10 kwa ajili ya ujenzi wa madrasa. Tunafanya haya kwa niaba ya Allah ili kujenga nyumba za kumuabudia na hii si mara ya kwanza mara nyingi nimekuwa nikichangia ujenzi wa msikiti huu,” amesema Bihimba.
Naye kiongozi wa msikiti huo, Sheikh Ramadhan Ally alisema “ tunashukuru leo tumepokea mzigo huu wa simenti kutoka kwa muumini mwenzetu. Tunashukuru tuko pamoja naye na tuko tayari kushirikiana naye katika ujenzi huu.
Leave a comment