Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bendera ya Chadema yawazuzua CCM Ukonga
Habari za SiasaTangulizi

Bendera ya Chadema yawazuzua CCM Ukonga

Spread the love

NI kama maneno ya kumnadi Mwita Waitara yamewaishia makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kwanza kushambulia rangi za bendera ya Chadema. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Livingstone Lusinde, Mbunge wa Mtera kupitia CCM ameishambulia rangi nyekundu iliyopo kwenye bendera hiyo akihoji maana yake.

Lusinde ametoa kauli hiyo leo tarehe 13 Septemba wakati wa kumnadi Waitara katika uchaguzi mdogo unaotarajia kufanyika tarehe 16 Septemba mwaka huu kwenye Jimbo la Ukonga jijini Dar es Salaam.

Lusinde amedai kuwa rangi nyekundu kwenye bendera ya Chadema haina uhalisia na kwamba rangi ya kijani ya CCM ina maana halisi.

“Mnawekaje bendera nyekundu, mlipigana vita wapi? Likipita gari la mzigo linaweka bendera nyekundu kwamba mzigo umezidi bodi sasa Chadema mzigo umezidi bodi vijana shukeni,” amesema.

Kwenye mkutano huo Lusinde amesema, Waitara anajua shida za wana Ukonga hivyo amewaomba wamchague ili ashirikiane na CCM kuzitatua.

Hata hivyo amesema, Waitara sio Mungu na hawezi kuzitatua zote kwani mwenye uwezo wa kutatua matatizo yote ni Mungu pekee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!