Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Chidawali atoa mbinu kupata viongozi waadilifu
Habari Mchanganyiko

Askofu Chidawali atoa mbinu kupata viongozi waadilifu

Spread the love

KANISA la Gospel Christ Church Tanzania (GCC) limetoa wito kwa jamii kuwajengea watoto misingi ya elimu na hofu ya Mungu ili kuwaandaa kuwa viongozi waadilifu wenye hofu ya Mungu na kupata Taifa lenye mafanikio ya kimaendeleo katika sekta mbalimbali. Anaripoti Danson Kaijage, Nairobi (endelea).

Wito huo umetolewa leo Jumanne na Mkuu wa Kanisa hilo Askofu Dk. Daud Chidawali wakati akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kutunukiwa Shahada ya Uzamivu ya masuala ya dini.

Shahada hiyo ametunukiwa na Chuo cha International Christian University of Ministry Education – Miissouri – USA tawi la Mombasa nchini Kenya.

Amesema bila ya viongozi bora hakuna maendeleo ya kimsingi kama vile ya kiroho, kielimu, kiuchumi, kiafya, kilimo na kijamii hivyo Taifa ni lazima wapatikane wenye kujali mahitaji ya watu ambayo ni ya msingi kwa wanadamu wake.

Dk. Chidawali amesema viongozi hao wanawajibu wa kutambua changamoto zinazowakabili wananchi wao juu ya maisha wanayoishi siku zote ikiwa ni haki yao ya msingi kama vile amani, ardhi, elimu, afya, malazi na chakula.

Hata hivyo, amesema ili Taifa liendelea linahitajika watu wasomi hivyo ninawaomba viongozi wa kidini na kiserikali kuhakikisha wanawaandaa vijana kielimu, ili nchi ipate viongozi watakaopewa dhamana ya kuongoza katika sekta mbalimbali.

“Hivyo niwaombe viongozi wawe wa kidini au kiserikali ni wajibu wetu kuhakikisha suala la elimu tunaliweka kipaumbele kwa watoto wetu kwa ajili ya kuwaanda ili waweze kushika nafasi katika sekta mbalimbali za uongozi,” amesema.

Amesema kuwa wakiandaliwa kwa kusomeshwa Taifa litaepukana na changamoto ya kuwapata viongozi wabovu wanaojijali wao wenyewe badala ya watu wote, pia wasiokuwa na maadili ya kiroho wapenda rushwa na wasiompenda Mungu kwa kuwa walio wengi watakuwa na tabia ya vitendo viovu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

DAWASA yatekeleza agizo la Samia kwa kutangaza zabuni kielektroniki

Spread the loveKiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Godfrey Mnzava...

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

error: Content is protected !!