WATU 22 wamefariki dunia huku zaidi ya 30 wakijeruhiwa katika ajali ya barabarani ikihusisha basi lenye namba za usajili T 732 ATH mali ya Kampuni ya AHMEED linalofanya safari zake kati ya Mbeya na Tanga kugongana uso kwa uso na lori lenye namba IT 2816 eneo la Melea kibaoni barabara ya Iringa-Morogoro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Fortunatus Muslim amesema, ajali hiyo imetolea Ijumaa ya tarehe 18 Machi 2022 saa 10 jioni wakati basi la Ahmed likitokea Mbeya kwenda Tanga kugongana na lori la lilikokuwa likisafiri kwenda nje ya nchi.
Amesema ajali imetokea wakati lori hilo likijaribu kumkwepa mwendesha pikipiki ndiyo likagongana na basi hilo, yakanasana na kusababisha vifo vya watu 13 papo hapo.
Nimesikitishwa na vifo vya watu 22 vilivyosababishwa na ajali ya basi kugongana na lori katika eneo la Melea Kibaoni, Morogoro. Nawapa pole wafiwa, nawaombea Marehemu wapumzike mahali pema na majeruhi wapone haraka. Nawasihi watumiaji wa barabara kuzingatia sheria za barabarani.
— Samia Suluhu (@SuluhuSamia) March 18, 2022
Katika ukurasa wake wa Twitter, Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameandika,”nimesikitishwa na vifo vya watu 22 vilivyosababishwa na ajali ya basi kugongana na lori katika eneo la Melea Kibaoni, Morogoro.”
“Nawapa pole wafiwa, nawaombea marehemu wapumzike mahali pema na majeruhi wapone haraka. Nawasihi watumiaji wa barabara kuzingatia sheria za barabarani.”
Leave a comment