Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Ajali yaua 22 Morogoro, Rais Samia awalilia
Habari MchanganyikoTangulizi

Ajali yaua 22 Morogoro, Rais Samia awalilia

Spread the love

 

WATU 22 wamefariki dunia huku zaidi ya 30 wakijeruhiwa katika ajali ya barabarani ikihusisha basi lenye namba za usajili T 732 ATH mali ya Kampuni ya AHMEED linalofanya safari zake kati ya Mbeya na Tanga kugongana uso kwa uso na lori lenye namba IT 2816 eneo la Melea kibaoni barabara ya Iringa-Morogoro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Fortunatus Muslim amesema, ajali hiyo imetolea Ijumaa ya tarehe 18 Machi 2022 saa 10 jioni wakati basi la Ahmed likitokea Mbeya kwenda Tanga kugongana na lori la lilikokuwa likisafiri kwenda nje ya nchi.

Amesema ajali imetokea wakati lori hilo likijaribu kumkwepa mwendesha pikipiki ndiyo likagongana na basi hilo, yakanasana na kusababisha vifo vya watu 13 papo hapo.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameandika,”nimesikitishwa na vifo vya watu 22 vilivyosababishwa na ajali ya basi kugongana na lori katika eneo la Melea Kibaoni, Morogoro.”

“Nawapa pole wafiwa, nawaombea marehemu wapumzike mahali pema na majeruhi wapone haraka. Nawasihi watumiaji wa barabara kuzingatia sheria za barabarani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!