Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yapuliza kipyenga uchaguzi viongozi kanda
Habari za Siasa

Chadema yapuliza kipyenga uchaguzi viongozi kanda

Maandamano Chadema
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeanza maandalizi ya uchaguzi wa viongozi wa kanda kwa kufungua dirisha la uchukuaji na urejeshaji fomu za kugombea nafasi hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana Ijumaa na Naibu Katibu Mkuu Chadema Bara, Benson Kigaila, zoezi la uchukuaji fomu za kugombea nafasi hizo katika kanda nne, Victoria, Serengeti, Magharibi na Nyasa, litafanyika kuanzia tarehe 12 hadi 22 Aprili mwaka huu.

Taarifa ya Kigaila imesema kuwa, uchaguzi wa viongozi wa kanda hizo utafanyika Mei 2024.

“Fomu za kuomba kugombea nafasi za uongozi ngazi ya Kanda husika zinapatikana Ofisi za Kanda, kwa Makatibu wa Mikoa na katika tovuti ya Chama kuanzia tarehe 12 Aprili 2024. Mwisho wa kurejesha fomu ni tarehe 22 Aprili 2024 saa 10:00 jioni katika Ofisi za Kanda husika ,” imesema taarifa ya Kigaila.

Nafasi zinazogombaniwa katika uchaguzi huo wa kanda ni mwenyekiti, makamu mwenyekiti, mweka hazina ngazi ya chama, pamoja na viongozi wa mabaraza ya Chadema ngazi ya kanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!