Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Biashara Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini
BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the love

SERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na gesi asilia baharini ambapo imeanza kutangaza utoaji wa leseni za uchimbaji na vitalu kwa wawekezaji. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 18 Machi 2024 na Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Shaaban Ali Othman, akitangaza uzinduzi wa duru ya kwanza ya zoezi la utoaji vitalu, utakaofanyika tarehe 20 Machi mwaka huu, visiwani humo.

Waziri huyo amesema uzinduzi huo unajiri baada ya zoezi la uchakataji data za ugawaji vitalu vipya vya maeneo ya bahari yaliyopo Mashariki mwa Zanzibar, kukamilika, pamoja na mabadiliko ya Sheria Namba 6 ya 2016 na mapitio ya modeli ya mkataba wa ugawaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia ya 2017.

“Nikiwa waziri mwenye dhamana ya mafuta na gesi asilia, nafurahi kuwajulisha maandalizi yanayohitajika ili Zanzibar kuanza kutoa vitalu vya wawekezaji kwa ajili ya utafutaji na uchimbaji mafuta na gesi asilia sasa imekamilika, ina maana kwamba sasa Zanzibar iko tayari kwa duru ya kwanza ya utoaji vitalu katika maeneo ya baharini kwa wawekezaji duniani kote,” amesema Othman.

“Hatua hii ya duru ya utangazaji vitalu itafungua fursa kwa wawekezaji zitakazopelekea kuimarika kwa uchumi wa Zanzibar pia kuiweka Zanzibar katika ramani ya dunia katika sekta ya mafuta na gesi asilia.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Expanse Tournament kasino mzigo umeongezwa hadi mil 400/=

Spread the love Jiunge na Meridianbet kasino kufurahia promosheni kubwaya Expanse Tournament,...

Biashara

Bounty Hunters sloti yenye utajiri Meridianbet kasino

Spread the love Congo DR inasifika sana kwa wingi wa madini ya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

error: Content is protected !!