Monday , 13 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mpango wa kuajiri mwanamke kushika mimba wafufuliwa
Habari MchanganyikoKimataifa

Mpango wa kuajiri mwanamke kushika mimba wafufuliwa

Spread the love

SERIKALI ya Thailand imepanga kufufua mpango wa wa biashara ya mwanamke kukubali kushika mimba na kujifungua mtoto kwa niaba ya familia fulani maarufu kama ‘Surrogacy’. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Mpango huo umerejea tena baada ya zoezi hilo kupigwa marufuku karibu muongo mmoja uliopita kutokana na mfululizo wa kashfa za usafirishaji haramu wa watoto na wanawake walioajiriwa kushika mimba hizo.

Mkuu wa idara inayotoa msaada wa huduma za afya katika Wizara ya Afya ya Umma nchini humo, Sura Visetsak ametangaza mpango huo mapema mwezi huu kwamba rasimu ya sheria ya kuhalalisha biashara hiyo imeshakamilika.

Amesema biashara hiyo “Surrogacy” itawahusu wanandoa wa ndani na wa nje ya Thailand kwa lengo la kuleta mageuzi yatakayobadili kiwango cha uzazi kinachopungua nchini humo. Hadi sasa nchi hiyo ina idadi ya watu milioni 71.

Hata hivyo, Sunwanee Dolah ambaye anatoa ushauri kwa makundi ya ndani kuhusu biashara ya binadamu na masuala ya haki za wanawake amesema bado kuna wasiwasi mkubwa kuhusu biashara hiyo.

“Huenda watu wengi watakuwa waathirika wa biashara ya usafirishaji binadamu, au watalazimika kutoa huduma hiyo kama biashara ya Surrogacy, itahalalishwa,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

NBC yazindua kadi uanachama msalaba mwekundu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Kimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

error: Content is protected !!