Monday , 13 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu aeleza Mzee Mwinyi alichomfanyia aliposhambuliwa na wasiojulikana
Habari za Siasa

Lissu aeleza Mzee Mwinyi alichomfanyia aliposhambuliwa na wasiojulikana

Spread the love

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, Tundu Lissu amesema aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili wa Tanzania, Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi, alikuwa mpole na mkarimu enzi za uhai wake. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Lissu ametoa kauli hiyo jana wakati akizungumzia kifo cha Mzee Mwinyi kilichotokea Alhamisi tarehe 29 Februari 2024.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, jana Jumapili, Lissu amesema Mzee Mwinyi pamoja na mke wake, Mama Sitti Mwinyi, walimtembelea hospitalini Nairobi nchini Kenya, alikokuwa anapatiwa matibabu baada ya kushambuliwa na risasi na watu wasiojulikana.

“Rais Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki dunia siku ya Alhamisi na kuzikwa jana (Jumamosi) alikuwa mpole na mkaribu. Nilipopigwa risasi Septemba 17 na kukimbizwa Nairobi kwa matibabu, Mzee Mwinyi na mama Sitti walikuwa Hospitali ya Nairobi kunitakia nafuu ya haraka. Apumzike kwa amani ya milele,” ameandika Lissu.

Lissu alilazwa hospitali jijini Nairobi Septemba 2017, baada ya kushambuliwa na risasi na watu wasiojulikana, nyumbani kwake Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!