Sunday , 12 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mhasibu Serengeti aswekwa rumande kwa madai ya kutafuna mil. 214
Habari za SiasaTangulizi

Mhasibu Serengeti aswekwa rumande kwa madai ya kutafuna mil. 214

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Spread the love

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwagiza Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, ACP Salum Morcase amkamate Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Saad Mutunzi Ishabailu kwa kosa la kuhamisha Sh. 214 kwa awamu nne. Anaripoti Mwandishi Wetu … ( endelea).

Amedai Mhasibu huyo amehamisha fedha hizo kwa njia ya uhamisho wa ndani kwa kushirikiana na watumishi wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI na kuzitumia kwa matumizi yao binafsi.

“Mkamate huyo bwana sasa hivi aende polisi akafunguliwe mashtaka, huyu ni wa kupeleka mahakamani moja kwa moja. DPP aelezwe afungue jalada la mashtaka.

“Wale wenzake tumewapeleka mahakamani tayari sababu tulibaini walihusika na wizi kama huu kwenye Manispaa ya Kigoma mwaka jana,” ameagiza Majaliwa.

Ametoa agizo hilo leo Jumanne jioni wakati akizungumza na madiwani na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kwenye kikao kilichofanyika katika kwenye Halmashauri hiyo, mkoani Mara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!