Monday , 13 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wahariri wamkaanga bosi bodi ya sukari kwa ububu
Habari za SiasaTangulizi

Wahariri wamkaanga bosi bodi ya sukari kwa ububu

Spread the love

Mkurugenzi Mkuu, Bodi ya Sukari Tanzania Prof. Kenneth Bengesi ameonja joto la jiwe kutoka kwa wahariri mbalimbali wa vyombo vya habari baada ya kumchongea mbele ya Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kwamba hapokei simu wala kujibu ujumbe mfupi wa maneno ‘meseji’ kutoka kwa waandishi wa habari wanapohitaji kupata ufafanuzi kuhusu masuala ya bodi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hayo yamejiri leo Alhamisi baada ya kuwasilisha taarifa ya hali ya sukari nchini ambapo pamoja na maswali aliyoulizwa, pia alihojiwa ni kwanini hapendi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya habari vinapohitaji ufafanuzi kutoka kwake.

Akijibu swali hilo, Profesa Bengesi alianza kujitetea kuwa mara nyingi huwa ‘bize’ na vikao lakini akasisitiza kuwa hutoa ushirikiano kwa kualikwa kwenye stesheni mbalimbali vya runinga na redio jambo ambalo lilionekana kupingwa na wahariri wengi.

Huku ming’ono ikiibuka pamoja na vicheko kutoka baadhi ya wahariri na waziri Bashe, hali hiyo iliyoonekana kumtia joto, Profesa huyo aliendelea kujitetea kuwa si kweli kwamba hatoi ushirikiano kwa vyombo hivyo.

Hayo yanajiri wakati Taifa likikabiliwa na uhaba wa sukari ambao Bashe amesema unatarajia kuanza kuisha kuanzia Machi mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wizara kutumia Sh. 3.5 bilioni kuchunguza afya ya akili, nguvu za kiume

Spread the loveWIZARA ya Afya, imepanga kutumia Sh. 3.50 bilioni, kwa ajili...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC yapaza sauti changamoto ya intaneti

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umeitaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Prof. Ndakidemi aitaka TMA kutoa taarifa kwa njia ya SMS

Spread the loveMBUNGE wa Moshi Vijijini, Profesa Patrick Ndakidemi (CCM) ameishauri Serikali...

error: Content is protected !!