Monday , 13 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mzee Mwinyi aendelea na matibabu chini ya uangalizi wa madaktari
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mzee Mwinyi aendelea na matibabu chini ya uangalizi wa madaktari

Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi
Spread the love

 

RAIS Mstaafu wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi, anaendelea kupatiwa matibabu chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari, huku familia ikiwaomba Watanzania wamuombee ili afya yake iimarike arudi kwenye hali ya kawaida. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Maendeleo ya afya ya Rais Mwinyi anayepatiwa matibabu kwa maradhi ya kifua, imetolewa jana Alhamisi na aliyekuwa katibu wake, Dk. Abdallah Makame, akizungumza na Kituo cha Televisheni cha Azam.

Dk. Makame alisema kwa sasa madaktari wanaomhudumia wameona hakuna haja ya kiongozi huyo kupelekwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

“Anaendelea kupata matibabu na baadhi ya wakati anakuwa na uangalizi wa karibu sana wa madaktari na wamesema kwamba wataendelea kumpa matibabu kwa hapa hakuna haja kwa sasa ya kumsafirisha labda kama watakuja kuona kuna haja ya kufanya hivyo,” alisema Dk. Makame na kuongeza:

“Na umri umesogea kidogo, mimi cha kusema tu tumuombee mzee wetu tumfanyie dua, tumuombee aweze kuimarika afya yake na aweze kutoka katika hali hiyo ya maradhi aungane na sisi tena tuendelee kupata faida kwake.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Vifo vitokanavyo na UKIMWI vyapungua

Spread the loveVIFO vinavyosababishwa na Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI), vimepungua kutoka...

AfyaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

NBC yazindua kadi uanachama msalaba mwekundu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

error: Content is protected !!