Monday , 13 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Familia ya Lowassa yafunguka, yamtaja Rais Samia
Habari za SiasaTangulizi

Familia ya Lowassa yafunguka, yamtaja Rais Samia

Spread the love

FAMILIA ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Hayati Edward Lowassa, imesema kiongozi huyo mstaafu alipigania uhai wake kabla ya mauti kumkuta. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumanne na Msemaji wa Familia ya Lowassa, Fredy Lowassa katika shughuli ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa mwanasiasa huyo aliyefariki dunia tarehe 10 Februari mwaka huu.

“Baba alipata umauti siku ya Jumamosi lakini kwa kweli tunasema tumelipokea hili kwa moyo wa imani kwasababu baba aligua muda mrefu, kama mlivyosema baba ni mpambanaji, kweli alipambana sana mpaka dakika ya mwisho lakini tunamshukuru Mungu na familia tumepokea kwa amani tunasema akapumzike kwa amani,” amesema Fredy.

“Kipekee naomba kutoa shukrani za familia kwa Rais Samia ukweli kama isingekuwa Rais Samia baba yetu asingefika hata hiyo Jumamosi. Mama Samia amekuwa ndugu, mlezi na mama mzazi kwetu kwa kweli hatuna cha kumlipa tunamshukuru sana. Siku anaondoka kuelekea Italia tayari hali ya baba ilikuwa imebadilika lakini alimtuma mkuu wa majeshi akawa anampa update kila baada ya nusu saa mpaka umauti unamkuta saa nane mchana,” amesema Fredy.

Amesema msiba huo sio wa ukoo wa Lowassa peke yake, bali wa taifa zima hasa wazazi na walezi ambao watoto wao wamesoma shule za sekondari za kata ambazo enzi za uhai wake akiwa Waziri Mkuu, Lowassa alisimamia ujenzi wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wizara kutumia Sh. 3.5 bilioni kuchunguza afya ya akili, nguvu za kiume

Spread the loveWIZARA ya Afya, imepanga kutumia Sh. 3.50 bilioni, kwa ajili...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC yapaza sauti changamoto ya intaneti

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umeitaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Prof. Ndakidemi aitaka TMA kutoa taarifa kwa njia ya SMS

Spread the loveMBUNGE wa Moshi Vijijini, Profesa Patrick Ndakidemi (CCM) ameishauri Serikali...

error: Content is protected !!