Monday , 13 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kero 22 kati ya 25 za Muungano zapatiwa ufumbuzi
Habari za Siasa

Kero 22 kati ya 25 za Muungano zapatiwa ufumbuzi

Spread the love

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dk. Selemani Jafo amesema tangu kuanzishwa kwa Kamati ya Pamoja ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SJMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) mwaka 2006, hoja 25 zimejadiliwa na kati ya hizo 22 tayari zimepatiwa na kuondolewa kwenye hoja za muungano. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Dk. Jafo ametoa kauli hiyo leo Ijumaa bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Najma Murtaza Giga (CCM) aliyetaka kujua mikakati ya Serikali ya kuhakikisha changamoto za Muungano ambazo hazijapatiwa ufumbuzi hazileti madhara nchini na lini zitapatiwa ufumbuzi.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dk. Selemani Jafo.

Akiendelea kujibu swali hilo, Dk. Jafo amesema SJMT na SMZ zimetengeneza utaratibu wa kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali za Muungano kupitia vikao vyake.

Amesema kuwa Serikali hizo mbili ziliunda Kamati ya Pamoja ya kutatua changamoto za Muungano ambayo huundwa na wajumbe kutoka pande zote mbili za Muungano.

Aidha, ameongeza kuwa hoja mbili zilizobaki katika orodha hiyo zipo katika hatua za kupatiwa ufumbuzi kupitia kamati hiyo inayoundwa na wajumbe kutoka SJMT na SMZ.

Aidha, Dk. Jafo amesisitiza kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali inayoongozwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi wana nia ya dhati ya kuzitafutia ufumbuzi hoja hizo mbili zilizobaki.

Kwa upande Giga ametoa pongezi kwa Serikali ya Awamu ya Sita kwa kutatua changamoto za Muungano na kuonesha imani kuwa zilizobaki zitatafutiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wizara kutumia Sh. 3.5 bilioni kuchunguza afya ya akili, nguvu za kiume

Spread the loveWIZARA ya Afya, imepanga kutumia Sh. 3.50 bilioni, kwa ajili...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC yapaza sauti changamoto ya intaneti

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umeitaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Prof. Ndakidemi aitaka TMA kutoa taarifa kwa njia ya SMS

Spread the loveMBUNGE wa Moshi Vijijini, Profesa Patrick Ndakidemi (CCM) ameishauri Serikali...

error: Content is protected !!