Saturday , 11 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto aukacha Urais, ataka kurudi bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Zitto aukacha Urais, ataka kurudi bungeni

Zitto Kabwe kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo
Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo anayemaliza muda wake, Zitto Kabwe amesema hatogombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama chake kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2025, bali atagombea ubunge wa Kigoma Mjini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Mwanasiasa huyo ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Februari 2024, akihojiwa na Kituo cha Televisheni cha Azam, baada ya kuulizwa kama atagombea urais au ubunge katika uchaguzi mkuu ujao.

Zitto amesema kwa vyovyote vile anataka kurejea bungeni ili auimarishe mhimili huo akidai Bunge limerudi nyuma tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.

“Wanachama wakinichagua kwamba niendelee (kumpitisha kuwa mgombea ubunge) nitagombea ubunge kwa sababu mimi kwa vyovyote vile nataka nirudi bungeni kwa sababu naamini kwamba miaka hii mitano ambayo hatukuwa bungeni Bunge limerudi nyuma,” amesema Zitto na kuongeza:

“ kuna matatizo kadhaa huwezi kulilaumu Bunge kwa ujumla wake lakini tunafahamu ni Bunge ambalo limetokana na mchakato wa uchaguzi ambao haukuwa wa kidemokrasia. Kwa hiyo tungependa kulirejesha Bunge lile kabla ya 2015 ili tuweze kutengeneza mazingira bora zaidi.”

Zitto amewahi kuwa mbunge wa Kigoma  katika vipindi tofauti ambapo 2005 alikuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT-Wazalendo, hadi 2020 aliposhindwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!