Sunday , 12 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wananchi walia ujenzi kituo cha afya kukwama kwa miaka 8
Afya

Wananchi walia ujenzi kituo cha afya kukwama kwa miaka 8

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Spread the love

Wananchi wa kijiji cha Songambele kilichopo kata ya Magamba wilayani Songwe mkoani humo, wameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa kituo cha afya Ileza ambacho ujenzi wake haujakamilika kwa miaka nane sasa.

Kituo hicho kilichoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi mwaka 2014, kinategemewa na wakazi 55,000 wa kata tano wanaolazimika kutembea umbali mrefu hadi Mkwajuni kupata huduma za tiba. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Wakizungumza leo Jumamosi na MwanaHALISI Online kwa nyakati tofauti wakazi wa eneo hilo la Magamba, wamesema ujenzi huo ulianza mwaka 2014 chini ya wilaya ya Chunya mkoani Mbeya kisha kuhamishiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Songwe mkoani Songwe.

Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Songwe, Secilia Kavishe akizungumza jambo na mganga mkuu kuhusu mradi wa kituo cha afya Magamba ofisini kwake.

Mmoja wa wakazi hao wa Songambele, Adam Mponzi amesema ujenzi wa kituo hicho uliendelezwa mwaka  2018 kwa kumalizia jengo ya huduma za nje (OPD) lililokuwa likijengwa kwa nguvu za wananchi tangu mwaka 2014.

“Tumeona serikali imeleta fedha ya kumalizia majengo mengi lakini bado mengine hayajakamilika licha ya huduma za nje zimeanza kutolewa lakini tunaomba majengo yakamilishwe tuepuke kutembea kilometa 72 kwenda wilayani kutibiwa,’’ amesema Mponzi.

Diwani wa kata hiyo, Kapala Makelele amesema kituo hicho kwa sasa kinategemewa na wakazi 55,000 wa kata 5 kwani mto Mtua ukijaa wananchi hawawezi kwenda upande wa pili kutibiwa.

Amesema amekaa kwenye nafasi ya udiwani tangu mwaka 1984 wakiwa chini ya wilaya ya Chunya na amedumu vipindi 8 hivyo anafahamu mazingira mabovu ya kata hizo hivyo ni vema mradi huo ukamaliziwa ili kuwapunguzia wananchi adha ya kupata matibabu.

Akizungumza kwa niaba ya Mganga mkuu, Mratibu wa afya uzazi na mtoto Dk. Lydia Kyumana amesema wananchi walianzisha ujenzi huo kwa thamani ya Sh 80 milioni kisha serikali ikatoa Sh 542 milioni ambazo zimewesha ujenzi wa mradi huo kufikia asilimia 98 huku huduma za nje (OPD) zianza kutolewa.

Aidha, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Cecilia Kavishe amesema kupitia mapato yao ya ndani wanatarajia kupeleka Sh. 135 milioni ili kukamilisha majengo yote yaliyosalia kwani dawa na vifaa tiba vimekwishapelekwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!