Sunday , 12 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwenyekiti CCM Arusha afariki dunia, Chongolo, Silaa wamlilia
Habari za SiasaTangulizi

Mwenyekiti CCM Arusha afariki dunia, Chongolo, Silaa wamlilia

Zelote Stephen
Spread the love

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha, Zelote Stephen amefariki dunia jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Katibu wa CCM mkoa Arusha, Mussa Matoroka amesema wamepata taarifa za kifo hicho leo jioni Alhamis tarehe 26 Oktoba 2023.

“Ni kweli Mwenyekiti amefariki jijini Dar es Salaam ambapo alikuwa amekwenda kupatiwa matibabu…huu ni msiba mkubwa kwetu CCM, familia ndugu na jamii,” amesema Matoroka.

Pia kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amendika katika akauti yake ya mtandao wa Instagram kuhusu taarifa za kifo cha kada huyo wa CCM na kuongeza kuwa mipango ya maazishi inafanywa nyumbani kwake Seaview Upanga jijini Dar es Salaam.

“Maziko yatafanyika nyumbani kwake Olasiti Arusha kwa tarehe itayotangazwa. Kwa kuwa ni ngumu kumtaarifu kila mmoja, naomba mpokee taarifa hii kwa wote. Tumwombee marehemu na tuiombee familia katika kipindi hiki cha msiba,” ameandika Silaa.

Aidha, katika ukurasa wake wa Instagram, Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo ameweka picha ya Marehemu Stephen huku akiandika maneno yanayoonyesha kuumizwa na kifo hicho.

“Taarifa za kuondokewa na Zelote Stephen, Mwenyekiti wetu wa CCM mkoa wa Arusha ni taarifa za kusikitisha sana. Kwani kwa hakika kifo chake kimetunyima fursa muhimu ya kuendelea kujifunza mengi na kuuishi uongozi wake”

“Mungu ameendelea kutufunza. Mipango yetu imekwama. Nenda Laigwanan. Nenda mzee wangu. Nilipokutembelea siku chache zilizopita hospitali ulinipa matumaini. Kumbe mipango ya Mungu ikabaki. Wewe ni shujaa, Nenda Kamanda”, imesomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Stephen kabla ya kuwa Mwenyekiti wa CCM mkoani Arusha, pia aliwahi kutumia nafasi mbalimbali ndani ya Serikali hususani Jeshi la Polisi ambako alikuwa Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma na Rukwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!