NYAMARI Ongegu anayejulikana zaidi kama Nyashinski ameahidi makubwa katika onyesho lake la kesho katika Tamasha kubwa la Serengeti Oktoba Festival litakalofanyika kesho tarehe 21 Oktoba, 2023 katika ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Tamasha hilo limeandaliwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries Ltd (SBL) kupitia bia yake ya Serengeti Lite litakuwa na burudani za kutosha ikiwa vinywaji lakini pia itatoa fulsa kujua tamaduni kutoka katika nchi hizo za Afrika Mashariki na Kati.
Nyashinski ambaye ni msanii wa Hip Hop kutokana nchini Kenya ametoa ahadi hiyo muda mchache mara baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere tayari kwa ajili tamasha hilo.
“Kesho ni siku kubwa sana kwangu, tangu nikiwa Kenya nilikuwa nafikiria na sikuamini kupata nafasi ya kupanda jukwaa moja na wasanii wakubwa kutoka Afrika Mashariki kama Ali Kiba na Jose Chameleone, mimi ni mshabiki mkubwa wa Chameleone hivyo kuwa naye katika jukwaa moja ni kitu kikubwa sana, alisema Nyashinski na kuongeza:
“Ali Kiba tulianza kitambo sana na nimekuwa nafuatilia nyimbo zake jambo lililonifanya niwe mshabiki wake mkubwa, hivyo itakuwa siku poa sana kushiriki naye kwenye jukwaa moja.”
Nyashinski alisema amejiandaa vya kutosha ikiwa kufanya mazoezi ya kwa ajili ya tamasha hilo, hivyo mashabiki wangu waje Coco Beach kwani watapata kitu bora zaidi.
Tamasha hilo mbali na burudani kutoka kwa wasanii wakubwa wa Afrika Mashariki, pia kutakuwa na tamaduni za nchi hizo pamoja na vyakula vya asili kutoka katika nchi hizo.
Leave a comment