Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Ujenzi shule ya kwanza kata ya Kilimani washika kasi
Elimu

Ujenzi shule ya kwanza kata ya Kilimani washika kasi

Spread the love

HATIMAYE kata ya Kilimani katika Jiji la Dodoma imeanza ujenzi wa shule ya msingi itakayogharimu kiasi cha Sh 80 milioni kwa kuanza na vyumba vinne vya madarasa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Ujenzi huo wa shule ya msingi unatokana na kata hiyo kutokuwa na shule ya msingi wala  sekondari tangu kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika.


Hali hiyo inatajwa kusababisha watoto kutembea umbali wa kilomita tatu kusaka elimu katika vijiji jirani.

Hata hivyo, leo tarehe 11 Oktoba 2023 Viongozi wa Kamati ya siasa ya  Chama Cha Mapinduzi Kata ya Kilimani Jijini Dodoma pamoja na Wajumbe wa  Sekretarieti   ya kata ya kilimani wamefanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa Shule  ya Msingi  unaotekelezwa katika Mtaa wa Chinyoyo.

Pamoja na kasi ya ujenzi huo  unaoendelea  viongozi hao wamesisitiza kasi katika ujenzi huo ili ukamilike kwa haraka na kwa wakati.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi kata ya kilimani, Nathani Chibeye amesema ujenzi huo wa shule ya msingi utakuwa mkombozi kwa kata ya kilimani na kuondoa adha ya watoto kutembea umbali mrefu kwenda shule za jirani.

Kwa upande wake Katibu wa CCM kata ya Kilimani, Rotta Ndimbo ameitaka kamati ya ujenzi na mkandarasi kuhakikisha wanatanguliza uzalendo katika ujenzi wa shule hiyo ili thamani ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi huo zitumike kama zilivyo kusudiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Waziri SMZ akoshwa na kazi za Global Education Link

Spread the loveSERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar SMZ imesema itaendesha msako na kuzifutia...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

error: Content is protected !!