Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya
HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the love

JESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad Slaa na Wakili Boniface Mwabukusi kufuatia kufanya mkutano wa hadahara ambao ulikuwa unadaiwa kwamba haukuwa na kibali, Anaripoi Kelvin Mwaipungu …(endelea)

Wito huo wa jeshi hilo ulitolewa jana, Oktoba 8, 2023 kwa njia ya barua mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo ambao ulifanyika kwenye kijiji cha Kandete, Halmashauri ya Busekelo.

Katika barua hiyo iliyotoka kwenye ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, iliwataka wawili hao kufika hii leo kwenye kituo Kikuu cha Polisi Mbeya majira ya saa 8, mchana kwa ajili ya mahojiano, kama sehemu ya upelelezi kwenye kesi hiyo.

Jana Video zilionesha Mwabukusi akiwa juu ya jukwaa akiwatangazia wananchi waliohudhuria kwenye mkutano huo kuwa Polisi wamefika viwanjani hapo kuzuia mkutano huo kwa sababu palipigwa nyimbo za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kwamba wenyewe wamelalamika kwa jeshi la Polisi.

“Polisi wanasema kuwa wamezuia kusanyiko hili eti kisa kumepigwa wimbo wa chadema hivyo wanataja tukakate rufaa kwa Waziri husika” alisikika Mwabukusi kwenye kipaza video hiyo

Endelea kutembelea MwanaHALISI Online kwa ajili ya kukujuza nini kinachoendelea  

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Bashiru Ally aivaa serikali kukalia vibali vya wahadhiri

Spread the loveMBUNGE wa kuteuliwa, Dk. Bashiru Ally amesema vikwazo vinavyoendekezwa na...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!