JAJI mmoja wa mahakama ya serikali mjini New York nchini Marekani ametupilia mbali juhudi za rais wa zamani wa nchi hiyo, Donald Trump za kuondolewa mashtaka ya ubakaji yaliyowasilishwa na mwandishi E, Jean Carroll, kwamba alimharibia jina kwa kupinga kwamba hakufanya hivyo katikati ya miaka ya 90. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Jaji Lewis Kaplan akiwa kwenye mahakama ya Manhattan, New York, amepinga ombi la Trump kwamba alikuwa analindwa dhidi ya mashtaka kutokana na cheo chake cha urais.
Trump alidai kwamba Carroll alisubiri kwa miongo kadhaa kabla ya kuwasilisha malalamiko yake hivyo ilimlazimu kujitetea.
Hata hivyo, Mawakili wa Trump na Carroll hawajasema lolote kutokana na uamuzi huo.
Carroll alifunguka mara ya kwanza hapo Juni 2019, pale aliposhtumu Trump kwamba alimshambulia kwenye chumba cha kujaribia mavazi kwenye duka la Bergdorf Goodman, kwenye kitongoji cha Manhattan.
Hata hivyo, Trump alikanusha kumfahamu na kusema kwamba Carroll hakuwa aina ya wanawake awapendao.
Carroll anaomba kulipwa ridhaa ya takriban dola Marekani milioni 10, na kesi yenyewe imepangwa kusikilizwa tarehe 15 Januari mwaka ujao.
Leave a comment