RAIS wa Kenya, William Ruto, naibu wake Rigathi Gachagua na Katibu Mkuu Mkuu, Musalia Mudavadi kuwa ni moja ya maafisa wa ngazi ya juu serikali ya nchi hiyo wanaoongoza kwa mishahara mikubwa katika nyongeza ya mishahara iliyopendekezwa hivi karibuni. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Tume ya Mishahara ya nchi hiyo (SRC) ilichapisha mapendekezo hayo kwenye kalenda yake kwa mwaka wa kifedha 2023/2024.
Kwa mujibu wa pendekezo la mishahara, maafisa wa serikali watasubiriwa ongezeko la asilimia 14 kuanzia tarehe 1 Julai 2023.
Aidha, kutokana na taarifa hiyo, tayari mjadala umeanza kushika kasi katika mitandao ya kijamii hasa ikizingatiwa serikali hiyo imekuwa ikilia kuwa na ukata wa fedha.
Baada ya kuchukua hatamu za uongozi, Naibu rais Rigathi Gachagua alisema walihidi kupunguza makali ya maisha kwa wananchi kwa kupunguza baadhi ya gharama zisizo za lazima Serikali.
Bloga maarufu nchini humo Pauline Njoroge ni miongoni mwa wale ambao wameanza kuikosoa serikali akisema Kenya Kwanza wameharibu uchumi na sasa wanataka kula zaidi.
Ikiwa pendekezo litapitishwa, Rais atapokea KSh 1.65 milioni (TSh. 28.3 milioni) kuanzia Julai 1, 2024.
Naibu Rais atapata KSh 1,367,438 (Tsh. 23.4 milioni), kutoka KSh 1,227,188 (Tsh 21 milioni) na ongezeko lingine hadi KSh 1.4 milioni (Tsh. 24 milioni) Julai 1, 2024, ambayo ni ongezeko la 14%.
Katibu Mkuu Mkuu Musalia Mudavadi na mawaziri wengine watapokea KSh 1,056,000, kutoka KSh 924,000, kuanzia Julai 1, 2023.
Leave a comment