JESHI la Urusi lililopo katika operesheni maalum nchini Ukraine limedai kuwaua majenerali wawili katika shambulizi la mapema wiki hii. Anaripoti Joseph Nyoni kwa msaada wa mitandao…(endelea).
Gazeti la The Moscow Times limeeleza kuwa, pamoja na kuwaua majenerali hao, majeshi ya Urusi pia yamedai kuwaua maafisa 50 wa jeshi la Ukraine.
Hali hiyo imeelezwa kuwa inaendelea kuipa mtihani Ukraine, nchi ambayo imekuwa ikielemewa na mashambulizi makali kutoka kwa majeshi ya Urusi huku majenerali na maafisa wake wakubwa wa jeshi wakizidi kupoteza maisha.
Shirika la habari la RIA liliripoti kwamba majenerali hao pamoja na maafisa 50 wa jeshi la Ukraine waliuawa katika mji wa Mashariki wa Kramatorsk nchini Ukraine tarehe 27 Juni mwaka huu.
Moscow pia imeeleza kuwa jaribio uasi lililofanywa na Wagner Yevgeny Prigozhin nchini Urusi halitaathiri operesheni za Urusi nchini Ukraine.
Leave a comment