Sunday , 12 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kiwango cha chini cha uhuru habari China chaongeza mashaka
Kimataifa

Kiwango cha chini cha uhuru habari China chaongeza mashaka

Spread the love

 

RIPOTI ya waandishi wa Habari wasiokuwa na mipaka duniani wanaosimamia tovuti ya ‘Just Earth News’ iliyotolewa mwezi Mei mwaka huu inaiweka China kuwa kwenye nafasi pili kwenye nchi zisizo kuwa na uhuru wa habari duniani ikizidiwa na Korea Kaskazini, Imeripotiwa na Business Standard …(endelea).

Ripoti hiyo kuwa waandishi wa habari na hata raia hawako salama ambapo wengine huchunguzwa na Chama tawala cha Kikomunisti cha China (CCP).

Tarehe 3 Mei inatambulika kimataifa kama Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, ukumbusho ulioanzishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 1993.

Azimio la Ulimwengu la Haki za Kibinadamu, lililoidhinishwa na UN, linakubali uhuru wa kujieleza kuwa haki ya msingi ambayo inaunda msingi wa kufurahia haki nyingine za binadamu.

Kuripoti ukweli ni gharama ndani ya China. Wakosoaji kama Fang Bin, Zhang Zhan, na Li Wenliang, ambao walifichua habari muhimu kuhusu janga la COVID katika hatua zake za awali, wanaendelea kuteswa wakiwa kizuizini na Serikali ya China.

Fang Bin, ambaye aliandika ukweli wa COVID-19, aliachiliwa kutoka gerezani Aprili 30 mwaka huu lakini anajikuta hawezi kurejea nyumbani kutokana na vitisho vilivyopokelewa na familia yake huko Wuhan. Bado Mamlaka zinamfuatilia Mwenendo wake.

Fung alifungwa kimyakimya hukumu ya kutumikia miaka mitatu jela tangu mwaka 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!