Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS
Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love

ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil United Front – Chama cha Wananchi (CUF) na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kati ya mwaka 2015 na Oktoba 2020, Maulid Mtulia, ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa wilaya (DAS). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mtulia aliyeondoka CUF katika kile kinachoitwa, “kuunga mkono juhudi,” amepelekwa wilayani Kakonko, mkoani Kigoma, kufanya kazi hiyo.

Katika orodha iliyotolewa na Ikulu ya Rais Samia Suluhu Hassan, jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi, tarehe 7 Juni 2023, jina la Maulidi Abdallah Mtulia, liko namba thelathini (30) kwenye orodha ya wateuliwa.

Maulidi Said Abdallah Mtulia, alitangaza kujiondoa CUF na kujiunga na CCM, tarehe 2 Desemba 2017. Alitangazwa tena kuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia CCM, tarehe 18 Feb 2018.

Kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe wakati anajiuzulu wadhifa huo, Mtulia alisema, atika barua yake ya kujiuzulu, Mtulia amesema amechukua maamuzi hayo, kwa utashi wake bila shinikizo la mtu yeyote.

Alisema, ameamua kujiuzulu nafasi yake hiyo ya ubunge na kuhama chama, kuwa kumetokana na uzoefu aliyoupata kwa miaka miwili ya ubunge.

Aliongeza, “nimebaini kuwa serikali ya CCM, ambacho ni chama tawala, inafanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani na imefanya vizuri katika mambo mengi ambayo sisi upinzani tuliahidi kuyatekeleza.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!