Tuesday , 26 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Kagame afumua tena Jeshi, awafuta kazi maofisa zaidi ya 200 wakiwemo majenerali
Kimataifa

Kagame afumua tena Jeshi, awafuta kazi maofisa zaidi ya 200 wakiwemo majenerali

Rais wa Rwanda Paul Kagame
Spread the love

 

RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amewafuta kazi Meja Jenerali Aloys Muganga, Brigedia Jenerali Francis Mutiganda, pamoja na maafisa wengine 14 wa Jeshi la Ulinzi la Rwanda (RDF). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Aidha, kiongozi huyo wa muda mrefu nchini Rwanda, ameidhinisha kutimuliwa kwa wanajeshi wengine 116 wenye nyadhifa mbalimbali na kuidhinisha kusitishwa kwa mikataba ya utumishi za wanajeshi 112 wa vyeo vingine, kwa mujibu wa taarifa ya RDF.

Taarifa hiyo haikutoa sababu ya kufutwa kazi kwa wanajeshi hao 244, iliyotangazwa mapema jana Jumatano.

Meja Jenerali Muganga, ambaye hadi anafutwa kazi alikuwa kamanda wa kitengo cha kiufundi, ni mhitimu wa Chuo cha Vita cha Marekani na aliwahi kuwa kamanda wa vikosi vya akiba vya Rwanda kutoka mwaka 2018 hadi 2019.

Brigedia Jenerali Mutiganda alikuwa mkuu wa usalama wa nje katika Huduma za Kitaifa za Ujasusi (NISS) hadi 2018 wakati Rais Kagame alipomhamisha tena katika makao makuu ya RDF katika mji mkuu Kigali.

Mabadiliko haya yakuja siku moja baada ya Rais Kagame, kufanya mabadiliko makubwa ya maafisa wakuu wa kijeshi.

Aidha, mabadiliko ya kuwafuta kazi vigogo hao yamekuja wakati ambapo mvutano umeongezeka kati ya Rwanda na jirani yake wa magharibi – Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ukizidi kushika kasi.

Ni baada ya serikali mjini Kinshasa, kuituhumu Rwanda kuchochea uasi mwake kwa kuwasaidia kundi la waasi la M23.

Katika mabadiliko yaliyotangazwa juzi, Kagame alimteuwa waziri mpya wa mambo ya ndani, mkuu mpya wa kijeshi, pamoja na mkuu mpya wa ujasusi. Juvénal Marizamunda, alitangazwa kuwa waziri mpya wa ulinzi wa Rwanda.

Naye Luteni Jenerali Mubarakh Muganga, alikabidhiwa jukumu la kuwa mkuu mpya wa majeshi (RDF).

 Bwana Marizamunda, ambaye kabla ya uteuzi huo, alikuwa mkuu wa jeshi la Magereza, amechukua nafasi ya Meja Jenerali Albert Murasira.

Kwa upande wake, Luteni Jenerali Muganga, alichukua nafasi ya Jenerali Jean Bosco Kazura, aliyekuwa kamanda mkuu wa jeshi la ardhini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

Kimataifa

Rais Kagame kuwania muhula wa nne

Spread the loveRais wa Rwanda, Paul Kagame amesema atawania muhula wa nne...

Kimataifa

Ukraine kufungua kituo cha nafaka Kenya

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto amesema serikali ya Ukraine inapanga...

Kimataifa

Kufungwa kwa mpaka wa Tibet kulivyoathiri maisha ya Wanepali katika vijiji vya milimani

Spread the love  KALU Dhami kutoka Dhalain moja ya kata ya Manispaa...

error: Content is protected !!