ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil United Front – Chama cha Wananchi (CUF) na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kati ya mwaka 2015 na Oktoba 2020, Maulid Mtulia, ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa wilaya (DAS). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Mtulia aliyeondoka CUF katika kile kinachoitwa, “kuunga mkono juhudi,” amepelekwa wilayani Kakonko, mkoani Kigoma, kufanya kazi hiyo.
Maulidi Said Abdallah Mtulia, alitangaza kujiondoa CUF na kujiunga na CCM, tarehe 2 Desemba 2017. Alitangazwa tena kuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia CCM, tarehe 18 Feb 2018.
U T E U Z I na U H A M I S H O wa Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji. pic.twitter.com/jCsjDg7qkW
— MwanaHALISI Digital (@Mwanahalisitz) June 7, 2023
Kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe wakati anajiuzulu wadhifa huo, Mtulia alisema, atika barua yake ya kujiuzulu, Mtulia amesema amechukua maamuzi hayo, kwa utashi wake bila shinikizo la mtu yeyote.
Alisema, ameamua kujiuzulu nafasi yake hiyo ya ubunge na kuhama chama, kuwa kumetokana na uzoefu aliyoupata kwa miaka miwili ya ubunge.
Leave a comment