Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini
KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Fulgence Kayishema
Spread the love

 

MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya Rwanda (1994), Fulgence Kayishema, amekamatwa nchini Afrika Kusini, baada ya msako wa zaidi ya miaka 20. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

 Vyanzo mbalimbali vya taarifa kutoka mashirika ya kimataifa ya habari, ikiwamo BBC, zinaeleza kuwa Kayishema, alikamatwa jana Jumatano katika mji wa Paarl, katika operesheni ya pamoja kati ya mamlaka za Afrika Kusini na timu ya Umoja wa Mataifa (UN).

Kulingana na shirika la UN linaloshughulikia kesi bora za uhalifu wa kivita kwa Rwanda na Yugoslavia – International Residual Mechanism for Criminal Tribunals’ (IRMCT) – Kayishema alikuwa mmoja wa watu waliotoroka baada ya kutenda uhalifu wa mauaji ya Kimbari na ambao wamekuwa wakitafutwa kwa udi na uvumba.

Alishtakiwa mwaka 2001 na Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), kwa makosa mbalimbali, ikiwamo mauaji ya halaiki, kushiriki katika mauaji ya halaiki, kula njama ya kutekeleza mauaji ya halaiki na uhalifu dhidi ya binadamu, pamoja na mauaji na uhalifu mwingine.

Anatuhumiwa kupanga mauaji ya takribani Watutsi 2,000 – wanawake, wanaume, watoto na wazee – katika kanisa moja lilipo wilayani Kivumu, ambapo alikuwa inspekta wa Polisi.

Aidha, Kayishema anatuhumiwa kushiriki moja kwa moja katika kupanga na kutekeleza mauaji hayo, ikiwa ni pamoja na kununua na kusambaza petroli ili kuchoma kanisa hilo pamoja na waliokuwa wanatafuta hifadhi katika nyumba hiyo ya ibada.

“Hili liliposhindikana, Kayishema na wenzake wengine, walitumia tingatinga kuangusha kanisa, kuwazika na kuwaua wakimbizi waliokuwemo ndani yake,” inaeleza sehemu ya hati yake ya mashitaka.

Kisha Kayishema na wenzake, “walisimamia uhamishaji wa maiti kutoka katika viwanja vya kanisa hadi kwenye makaburi ya pamoja kwa takriban siku mbili zilizofuata,” taarifa ya IRMCT imeeleza.

Mshukiwa ambaye amekuwa akitoroka tangu kufunguliwa mashitaka, anatazamiwa kufikishwa katika mahakama ya Cape Town siku ya Ijumaa, ripoti zinasema.

Takriban watu karibu 800,000 waliuawa pale waasi wa Kihutu wenye msimamo mkali walipowauwa Watutsi na Wahutu wenye msimamo wa kati, katika muda wa siku 100, kuanzia kuuliwa kwa marais Juvenal Habyarimana wa Rwanda na Cyprien Ntaryamira wa Burundi tarehe 6 Aprili hadi katikati ya Julai 1994.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!