Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti
Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Dk. Lazaro Mambosasa
Spread the love

 

JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na mabadiliko ya sayansi na technolojia limepanga kuja na mkakati wa Pamoja kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika maswala ya tafiti mbalimbali ambazo zimelenga kubaini na kukomesha vitendo vya kiharifu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akiongea na waandishi wa Habari Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi , SACP Dk. Lazaro Mambosasa amesema moja ya majukumu yao ni kulinda rai ana mali zao ambapo amebainisha kuwa kupitia kitengo cha utafiti ndani ya Jeshi hilo na katika chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam wameona vyema wafike chuoni hapo ili kujifunza maswala mbalimbali katika tafiti.

Aidha SACP Dk. Mambosasa amewambia waandishi kuwa malengo ya Mkuu wa Jeshi hilo IGP Camillus Wambura ni kuona Jeshi la Polisi linawekeza katika tafiti ambapo amebainisha kuwa Jeshi hilo limepanga kuingia makubaliano baina ya chuo cha taaluma ya Polisi Dar es salaam Pamoja na chuo kikuu cha Dar es salaam katika kufanya tafiti.

Nae Kamishina Msaidizi wa Polisi ACP Ralph Meela ambae ni Mkuu wa Kituo cha Utafiti cha Jeshi la Polisi kilichopo Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam amesema kuwa kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia wameona vyema waje na mtazamo mpya katika kutanzua mbinu zinazotumiwa na wahalifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!