Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wamuaga rasmi IGP Mstaafu, Balozi Simon Sirro
Habari Mchanganyiko

Polisi wamuaga rasmi IGP Mstaafu, Balozi Simon Sirro

Spread the love

JESHI la Polisi Tanzania, limemuaga rasmi IGP Mstaafu, Balozi Simon Sirro leo tarehe 10 Mei  2023 baada ya kustaafu Utumishi ndani ya Jeshi la Polisi kwa mujibu wa sheria Machi 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Sherehe za kumuaga Sirro zimefanyika Chuo cha Taaluma ya Polisi Dares Salaam – DPA, kilichopo Kurasini Jijini Dar es Salaam kwa gwaride maalum kama utaratibu wa Jeshi unavyoelekeza wa gwaride maalum la Viongozi wa Polisi waliofikia cheo cha Kamishna wa Polisi na Inspekta Jenerali wa Polisi.


IGP Mstaafu, Balozi Simon Nyakoro Sirro amelitumika Jeshi la Polisi kwa miaka 30 tangu Februari 19, 1993 alipojiunga rasmi hadi kustaafu mwezi Machi, 2023 akiwa ni Mkuu wa Jeshi la Polisi wa 10 tangu uhuru wa 1961 akiongoza kuanzia Mei 28, 2017 hadi tarehe 20 Julai 2022.

Wengine waliowahi kushika nyadhifa hiyo ni ya ukuu wa Jeshi la Polisi ni IGP Mstaafu wa kwanza nchini, Elangwa Shaidi (1964 -1970), Hamza Azizi (1970 – 1973), Samweli Pundugu (1973- 1975), Philemon Maya (1975-1980), Solomon Liani (1980 – 1984), Harun Mahundi (1984-1996) Omari Mahita (1996 – 2006), Saidi Mwema (2006-2013) na IGP Mstaafu Ernest Mangu (2013-2017).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!