Sunday , 12 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Uganda auawa na mlinzi wake
Kimataifa

Waziri Uganda auawa na mlinzi wake

Charles Okello Engola
Spread the love

 

MWANAJESHI wa Jeshi la Uganda amempiga risasi na kumuua waziri katika Serikali ya Uganda ambaye alikuwa akimlinda.

Kanali mstaafu Charles Okello Engola, ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Kazi, alipigwa risasi nyumbani kwake katika mji mkuu, Kampala leo Jumanne asubuhi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa.

Haijajulikana wazi iwapo kulikuwa na mabishano kati yake na mkuu wake, kabla ya kumpiga risasi.

Baadhi ya mashahidi walisema askari huyo alizunguka kwenye maeneo jirani akifyatua risasi hewani.

Hatimaye mwanajeshi huyo, ambaye hajatambuliwa rasmi, alijipiga risasi na kufa dakika chache baadaye.

Taarifa zinasema kuwa watu kadhaa wamejeruhiwa katika tukio hilo.

Video kwenye mitandao ya kijamii inaonyesha wenyeji wa eneo hilo wakikusanyika katika eneo la tukio kwa mshituko.

Kanali Engola awali alihudumu kama Naibu Waziri wa Ulinzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!