Tuesday , 14 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Tumebeba ‘teaching allowance’
Habari za Siasa

Rais Samia: Tumebeba ‘teaching allowance’

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema suala la posho ya kufundishia (teaching allowance) kwa walimu ni mzigo mkubwa kwenye kapu la serikali hivyo atakwenda kuangalia uwezo wa nchi na kuona atafanya nini. Anaripoti Gabriel Mushi, Morogoro … (endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo baada ya Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Tumaini Nyamuhokya kumuomba kuwarejeshea walimu mpango wa posho hiyo ambayo imesitishwa kwa muda mrefu.

“Mabango ni mengi lakini kuna neno dogo limekuwa likinipa shida kwenye mabango hayo ya walimu… linaitwa teaching allowance, wameweka kwenye mabango yao.

“Ilikuwepo siku za nyuma lakini katikati kikapotea na kufifia, leo wametukumbusha, ikikupendeza usisahau watumishi walimu katika hilo,” amesema Rais Nyamhokya wakati akitoa hotuba ya kumkaribisha Rais Samia kuhutubia katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani leo tarehe 1 Mei 2023.

Aidha, Rais Samia ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo yaliyofanyika kitaifa katika uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro, amesema suala hilo amelibeba.

“Suala la teaching allowance tumelichukua, unajua walimu na sekta ya afya ni jeshi kubwa, kwa hiyo allowance za walimu hata zikiwa ndogo ukiweka kwa pamoja ni mzigo mkubwa kwenye kapu la serikal hivyo tutakwenda kuangalia uwezo wa nchi alafu tuone tutafanya nini lakini tumelibeba,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wizara kutumia Sh. 3.5 bilioni kuchunguza afya ya akili, nguvu za kiume

Spread the loveWIZARA ya Afya, imepanga kutumia Sh. 3.50 bilioni, kwa ajili...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC yapaza sauti changamoto ya intaneti

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umeitaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Prof. Ndakidemi aitaka TMA kutoa taarifa kwa njia ya SMS

Spread the loveMBUNGE wa Moshi Vijijini, Profesa Patrick Ndakidemi (CCM) ameishauri Serikali...

error: Content is protected !!