Monday , 13 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Israel yashambulia Lebanon, Gaza baada yakushambuliwa kwa roketi
Kimataifa

Israel yashambulia Lebanon, Gaza baada yakushambuliwa kwa roketi

Spread the love

 

JESHI la Israel limesema kuwa limeshambulia maeneo yenye uhusiano na kundi la wapiganaji wa Palestina Hamas ndani ya Lebanon na katika Ukanda wa Gaza. BBC imeripoti … (endelea).

Mashambulizi hayo yanakuja baada ya shambulio kubwa la roketi dhidi ya Israel kutoka Lebanon, ambalo Waisraeli walilaumu kundi la Hamas.

Jeshi la Ulinzi la Israel lilisema miundombinu ya “kigaidi” ya Hamas ilipigwa kusini mwa Lebanon.

Hali ya wasiwasi imetanda baada ya polisi wa Israel kuvamia msikiti wa Al-Aqsa mjini Jerusalem usiku mtawalia mapema wiki hii.

Msikiti huo ni eneo la tatu takatifu kwa Uislamu, na uvamizi wa Israel umezusha makabiliano makali na Wapalestina ndani na kusababisha hasira katika eneo hilo kubwa.

Mkuu wa Hamas Ismail Haniyeh, ambaye alikuwa Lebanon wakati roketi hizo ziliporushwa, alisema Wapalestina “hawataketi wakitazama tu” uvamizi wa Israel ukiendelea.

Katika taarifa mapema siku ya Ijumaa, IDF iliandika kwenye Twitter kwamba ilikuwa imejiwekea melenga ya mahali pa kushambilia “ikiwa ni pamoja na miundombinu ya kigaidi ya Hamas kusini mwa Lebanon”.

IDF iliongeza kuwa haitaruhusu Hamas kufanya kazi kutoka Lebanon na kushikilia Lebanon “kuwajibika kwa kila moto ulioelekezwa kutoka katika eneo lake”.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!