Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa
Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

UONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan zimeongeza ari kubwa kwa wachezaji kuipigania timu yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamesemwa na Mratibu wa Yanga, Hafidh Salehe, wakati wa uchezeshaji wa droo ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam hatua ya robo fainali, iliyofanyika jana katika ofisi za Azam Media.

Salehe alisema kipindi cha nyuma timu yao ilikuwa inaishia hatua ya awali ya michuano ya Kimataifa, lakini sasa vijana wamekuwa na hamasa kubwa ya kuipigania nembo ya timu yao.

“Sisi kwa sasa tunashukuru kwa hamasa hii, unawaona kabisa wachezaji wanavyopambana ili kuipatia timu matokeo mazuri uwanjani, hivyo tunashukuru kwa kila kitu kinachochangia ushindi wetu.

“Historia imebadilika na wakati huu tunaenda kwenye mechi ya mwisho wa wiki tukiwa na shauku kubwa ya kuona timu yetu inashinda mbele ya wageni wetu US Monastir, mchezo utakaopigwa siku ya Jumapili katika Uwanja wa Taifa wa Benjamini Mkapa, jijini Dar es Salaam,” alisema.

Yanga na Simba wanaogelea bahari ya fedha za Rais Samia aliyeahidi kununua kwa Sh Milioni 5, kila goli linalopatikana kwa timu hizo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!