Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Watanzania watakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ili kuongeza mapato
Habari Mchanganyiko

Watanzania watakiwa kutembelea hifadhi za Taifa ili kuongeza mapato

Watalii wakiwa moja ya mbuga nchini Tanzania
Spread the love

WATANZANIA wametakiwa kujenga utamaduni wa kufanya utalii wa ndani ili kuinua pato la Taifa ikiwa ni pamoja na kujivunia rasilimali muhimu za nchi zilizopo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma( endelea).

Ushauri huo umetolewa leo tarehe 16 Machi 2023 na Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la uhifadhi TANAPA, Ofisi ya kiunganishi Dodoma, Dk. Noelia Myonga alipozungumza na waandishi wa habari juu ya umuhimu wa uhifadhi.

Dk. Noelia amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na vivutio vingi ambavyo ni muhimu kuvitembelea na bahati mbaya zaidi watanzania waliowengi bado hawana mwamko wa kutembelea vivutio hivyo.

Amesema kwa sasa Tanzania ina hifadhi 22 ambazo kila hifadhi inamvuto wake na maajabu yake ambayo yanawavutia watalii kwa kufika na kujifunza mambo kadhaa.

Amezitaja hifanyi hizo kuwa ni Arusha, Burigi -Chato, Gombe, Ibanda -Kyerwa, Katavi, Kigosi, Kilimanjaro, Kisiwa cha Rubondo, Kisiwa cha Saanane, Kitulo, Manyara, Mikumi, Mhale, Uduzungwa, Mkomazi, Mto Ugala, Nyerere, Ruaha, Rumanyika Karagwe, Saadani, Serengeti na Tarangire.

“Kila hifadhi imekuwa na mvuto wake tofauti kabisa, mfano hifadhi ya Manyara kuna simba ambao wanapanda miti na ndege wazuri na waajabu, hifadhi ya Tarangire kuna tembo wengi na mibuyu mikubwa ambayo inavutia zaidi, hifadhi ya Saadani kuna kasa wakubwa na wa kijani na vivutio vingi katika hifadhi mbalimbali” ameeleza Dk. Noelia.

Pia amesema kuna utalii wa kihistoria jambo ambalo linaonekana kusahaulika huku akikumbushia sehemu za Kondoa Irangi, Kongwa kwenye sehemu za wapigania uhuru.

Anatoa mfano wa eneo la Kongwa ambalo kuna kisa cha tembo aliyezama katika kisima cha maji na kusababisha Dodoma kupewa jina hilo.

Aidha, amesema kuwa TANAPA kwa sasa wameanzisha vikundi vya hamasa pamoja na kutoa elimu kwa wanafunzi ili kuona umuhimu wa kuwafundisha umuhimu wa uhifadhi na faida zake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!