Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Mwamakula alilia uhuru wa vyombo vya habari
Habari Mchanganyiko

Askofu Mwamakula alilia uhuru wa vyombo vya habari

Kiongozi wa Kanisa la Uamsho la Moravian, Askofu Emmaus Mwamakula
Spread the love

 

ASKOFU wa Kanisa la Uamsho la Moravian, Emmaus Mwamakula, madai ya upatikanaji katiba mpya, yanatakiwa yaende sambamba na uimarishwaji wa uhuru wa vyombo vya habari, ili visitumike ama kuminywa na vyama vya siasa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Askofu Mwamakula ametoa kauli hiyo hivi karibuni, akihojiwa na MwanaHALISI Online na Tv, jijini Dar es Salaam.

“Miaka saba iliyopita vyombo vingi vya habari vilizimia, vingine vikawa mahututi, vingine vilipona na vilivyopona wakawa waoga kweli kweli. Katika ukombozi unaodaiwa sasa hivi wa katiba utaenda pamoja na uhuru wa vyombo vya habari ili visiweke mfumo na chama tawala au vyama vya siasa,” alisema Askofu Mwamakula.

Kiongozi huyo wa dini amesema, vyombo vya habari ni jicho na sikio la umma na nchi kwa ujumla, kwa kuwa vinafanya kazi inayogusa makundi yote iikiwemo Serikali.

“Kwa sababu hiyo chombo cha habari tukione kwamba ni mtumishi wa wote katika nchi, hakiko pale kwa ajili ya kufurahisha kundi fulani, hakiko kwa ajili ya Serikali wala chama tawala, upinzani au vyombo vya dini. Viko kwa ajili ya jamii yote kwa ujumla,” alisema Askofu Mwamakula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!