Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Mwamakula alilia uhuru wa vyombo vya habari
Habari Mchanganyiko

Askofu Mwamakula alilia uhuru wa vyombo vya habari

Kiongozi wa Kanisa la Uamsho la Moravian, Askofu Emmaus Mwamakula
Spread the love

 

ASKOFU wa Kanisa la Uamsho la Moravian, Emmaus Mwamakula, madai ya upatikanaji katiba mpya, yanatakiwa yaende sambamba na uimarishwaji wa uhuru wa vyombo vya habari, ili visitumike ama kuminywa na vyama vya siasa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Askofu Mwamakula ametoa kauli hiyo hivi karibuni, akihojiwa na MwanaHALISI Online na Tv, jijini Dar es Salaam.

“Miaka saba iliyopita vyombo vingi vya habari vilizimia, vingine vikawa mahututi, vingine vilipona na vilivyopona wakawa waoga kweli kweli. Katika ukombozi unaodaiwa sasa hivi wa katiba utaenda pamoja na uhuru wa vyombo vya habari ili visiweke mfumo na chama tawala au vyama vya siasa,” alisema Askofu Mwamakula.

Kiongozi huyo wa dini amesema, vyombo vya habari ni jicho na sikio la umma na nchi kwa ujumla, kwa kuwa vinafanya kazi inayogusa makundi yote iikiwemo Serikali.

“Kwa sababu hiyo chombo cha habari tukione kwamba ni mtumishi wa wote katika nchi, hakiko pale kwa ajili ya kufurahisha kundi fulani, hakiko kwa ajili ya Serikali wala chama tawala, upinzani au vyombo vya dini. Viko kwa ajili ya jamii yote kwa ujumla,” alisema Askofu Mwamakula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!