Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Dk. Mwinyi ateua viongozi
Habari za Siasa

Rais Dk. Mwinyi ateua viongozi

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, leo Jumatano, tarehe 16 Novemba 2022, amefanya uteuzi wa viongozi wawili, akiwemo Dk. Sharifa Omar Salim, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Ununuzi na Uondoshaji wa Mali za Umma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Mhandisi Zena Said.

“Dk. Sharifa ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Ununuzi na Uondoshaji wa Mali za Umma. Dk. Sharifa ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA),” imesema taarifa ya Mhandisi Zena.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kiongozi mwingine aliyeteuliwa ni Dk. Hashim Hamza Chande, kuwa Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Mipango, Fedha na Utawala katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA). Kabla ya uteuzi huo, Dk. Hashim alikuwa Mkuu wa Skuli ya Kilimo, Kizimbani SUZA.

“Uteuzi huo unaanza leo tarehe 16 Novemba 2022,” imesema taarifa ya Mhandisi Zena.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!