Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Dk. Mwinyi ateua viongozi
Habari za Siasa

Rais Dk. Mwinyi ateua viongozi

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, leo Jumatano, tarehe 16 Novemba 2022, amefanya uteuzi wa viongozi wawili, akiwemo Dk. Sharifa Omar Salim, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Ununuzi na Uondoshaji wa Mali za Umma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Mhandisi Zena Said.

“Dk. Sharifa ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Ununuzi na Uondoshaji wa Mali za Umma. Dk. Sharifa ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA),” imesema taarifa ya Mhandisi Zena.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kiongozi mwingine aliyeteuliwa ni Dk. Hashim Hamza Chande, kuwa Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Mipango, Fedha na Utawala katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA). Kabla ya uteuzi huo, Dk. Hashim alikuwa Mkuu wa Skuli ya Kilimo, Kizimbani SUZA.

“Uteuzi huo unaanza leo tarehe 16 Novemba 2022,” imesema taarifa ya Mhandisi Zena.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!