Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kilango aanzisha miradi kusaka kura Serikali za mitaa
Habari za Siasa

Kilango aanzisha miradi kusaka kura Serikali za mitaa

Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango
Spread the love

 

MBUNGE wa Same Mashariki, Anne Kilango (CCM) ameazisha miradi ya viti vya kukodisha kwa ajili ya biashara kwenye kata 14 katika jimbo lake la Same Mashariki ambazo kila kata zimepatiwa viti 100. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Amesema atahakikisha pesa zinazopatikana zinawasaidia kwenye kampeni za wenyeviti wa vitongoji na vijiji ifikapo mwaka 2024 kusiwe na changamoto yoyote ya pesa wakati wa kampeni.

Pia amewagiza madiwani kutunza mradi huo wa kukodisha viti hili huwe chachu ya maendeleo katika serikali za mitaa lengo ni kuwanadi vingozi wao wa chama cha mapinduzi

Kilango amesisitiza kata itakayofanya vizuri 2023 atawaongezea mradi mwingine ili wajikite kutengeneza pesa ambazo zitawanufaisha kwenye chaguzi ndogo ndogo na kuondoka na dhana za kuomba pesa za kampeni.

Alisema moja ya malengo ya kuanzisha miradi hiyo ni kukisaidia CCM kutekeleza Ilani kushinda chaguzi zote za serikali ya mtaa na uchaguzi mkuu ambao utafanyika Agosti 2025

Pamoja na mambo mengine, Mbunge huyo ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za kutosha kwa ajili ya ujenzi wa barabara za Same Mashariki ambazo sasa zimekabidhiwa wakandarasi na zinafanyiwa kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!