Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ruto, Kenyatta wakutana mara ya kwanza baada ya uchaguzi
KimataifaTangulizi

Ruto, Kenyatta wakutana mara ya kwanza baada ya uchaguzi

Spread the love

RAIS mteule William Ruto leo Jumatatu tarehe 12 Septemba, 2022, amekutana na rais anayeondoka madarakani Uhuru Kenyatta katika Ikulu ya Rais Jijini Nairobi. Anaripotui Mwandishi Wetu…(endelea)

Ruto aliwasili katika Ikulu ya rais saa kumi na kupokewa na mwenyeji wake Uhuru Kenyatta. Rais Mteule aliambatana na mkewe Rachel Ruto.

Hii ni mara ya kwanza kwa wawili hao kukutana tangu Wakenya waliposhiriki katika shughuli ya kupiga kura ili kumchagua rais mpya.

Wawili hao walitofautiana baada ya rais Uhuru Kenyatta kumuunga mkono kiongozi wa upinzani Raila odinga katika uchaguzi uliopita.

Mkutano wao unajiri siku moja kabla ya sherehe ya kumuapisha William Ruto kuwa rais mpya wa Kenya.

Takriban viongozi 20 wa mataifa mbalimbali wamethibitisha kuhudhuria sherehe hiyo hapo kesho Jumanne akiwemo rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Ruto aliibuka mshindi katika uchaguzi wa urais baada ya kumshinda mpinzani wake Raila Odinga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

error: Content is protected !!